Mwimbaji wa Nigeria 2 Face Idibia ambaye wengine humuita dume la mbegu kutokana na kuwa na watoto saba, hivi sasa hataki tena jina hilo lililompa umaarufu.
Taarifa rasmi kwa vyombo vya habari iliyotolewa na timu yake imeeleza dhahiri jina jipya la mwimbaji huyo.
“Kiwanda cha burudani kimeshuhudia mabadiliko mapya leo wakati mshindi wa tuzo kadhaa, 2Face Innocent Idibia hivi sasa amejipa jina jipya la jukwaani kuwa ni 2Baba,” imeeleza taarifa hiyo.