Hatimaye Tanzania imepangiwa kundi katika michuano ya Kombe la Mataifa Huru Barani Afrika (AFCON), huku ikiangukia kwenye kundi C na kufanikiwa kumkwepa mwenyeji.
Katika mchakato wa kupanga makundi uliofanyika jana usiku jijini Cairo, katika kundi hilo Tanzania imengwa pamoja na Algeria, Kenya na Senegal.
Upangaji wa makundi ulifanyika kutokana na ‘Ports’ 4 zilizokuwepo, ambapo kila port ilitoa timu moja ili kuzalisha kundi lenye timu nne. Viwango vya FIFA na CAF vikitumiwa kama vigezo vya kupata timu za kila port.
Kila timu iliyokuwa Port1 iliongoza kundi kisha ikaongezewa timu kutoka port 2-4. Tanzania iliyokuwa kwenye Port 4 ilifanikiwa kumkwepa mwenyeji na kujiunga na jirani zake Kenya pamoja na timu za Algeria na Senegal.
Mashindano ya AFCON yanatarajiwa kuanza Juni mwaka huu. Angalia makundi yote hapa:
Kundi A:
 Egypt
 DR Congo
 Uganda
 Zimbabwe
Kundi B:
NigeriaÂ
GuineaÂ
MadagascarÂ
BurundiÂ
Kundi C:
 Senegal
 Algeria
 Kenya
 Tanzania
Kundi D:
 Morocco
 Ivory Coast
 South Africa
 Namibia
Kundi E:
 Tunisia
 Mali
 Mauritania
 Angola
Kundi F:
 Cameroon
 Ghana
 Benin
 Guinea-Bissau