Alan Ruschel, aliyesalimika kwenye ajali ya ndege iliyoua watu zaidi ya 70 wakiwemo wachezaji wa timu ya Chapecoense ya Brazil ameanza kutembea.
Ruschel ameanza kutembea kwa msaada wa mmoja wa madaktari na amewatumia salami mashabiki wa Chape na familia yake kwamba anaendelea vizuri.
Beki huyo wa Chape amekuwa akiendelea kupata matibabu baada ya kuvunjika mifupa kadhaa mwilini mwake.
Wakati Ruschel anaendelea matibabu katika Kliniki ya Somer Clinic katika mii wa Rionegra, Colombia, miili ya wachezaji wa Chape ilirejeshwa Brazil kwa ajili ya mazishi.
Walipata ajali wakiwa njiani kwenda Medellin nchini Colombia kucheza mechi ambayo mwisho, imeamuliwa timu hiyo ipewe ubingwa.

JKU Kumjaribu George Lwandamina
Jaribio La Kuzuia Mkutano Wa Simba Lakwama