Hatimaye kiungo anayehusishwa kujiunga na Young Africans, Fabrice Mugheni, amewaaga rasmi mashabiki wa timu yake ya Rayon Sports ya Rwanda kwa kuwaambia ataondoka mwishoni mwa msimu huu.

Fabrice raia wa DR Congo aliwahi kusema kuwa, aliombwa video zake na Injinia Hersi Said ambaye ni Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM ambaye pia anahusika na masuala ya usajili ndani ya Young Africans.

Fabrice kupitia mtandao wake wa Instagram, aliwaaga rasmi mashabiki wa timu hiyo jambo ambalo linatafsiriwa kama huenda akawa alishamalizana na Young Africans kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo.

Young Africans wamekua wanahusishwa na mipango ya usajili wa baadhi ya wachezaji wa kimataifa, hii ni kwa ajili ya kujipanga vyema kwa msimu ujao wa Ligi Kuu na michuano ya kimataifa, endapo watapata fursa ya kuiwakilisha nchi kupitia michuano ya Kombe La Shirikisho.

RAIS NKURUNZIZA: Kocha aliyehukumiwa kifo akaangukia URAIS, vita na mapenzi - Makala
Waziri Mpango aishukuru IMF kuisamehe Tanzania deni la Bilioni 33