Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel anatarajiwa kuhudhuria mchezo wa kirafiki dhidi ya Uholanzi usiku wa leo ambao utafanyika kama ulivyopangwa licha ya timu hiyo kuwa bado katika mshangao wa mashambulizi ya mauaji jijini Paris. 

Msemaji wa serikali amesema Merkel anatarajia kuwepo uwanjani kwa ajili ya mchezo huo utakaofanyika huko Hanover sambamba na waziri wa mambo ya ndani Thomas de Maiziere. 

Mabingwa hao wa dunia walikuwa wakicheza na Ufaransa huko Paris Ijumaa iliyopita wakati mashabulizi yalipotokea katika viunga kadhaa vya mji huo na kusababisha vifo vya watu 129. 

Rais wa muda wa Shirikisho la Soka la Ujerumani-DFB, Reinhard Rauball amesema kikosi cha timu hiyo kinataka kupeleka ujumbe kuwa hawatatishwa wala kukubali kuendeshwa na magaidi.

Game Ya Ubelgiji Vs Hispania Yaota Mbawa
Stars Kutajirishwa Kama Wataing'oa Algeria