Askari mmoja  wa Chuo cha Mafunzo ya Wafungwa cha Losperfontein, nchini Afrika Kusini amejinyonga hadi kufa mara baada ya kuzagaa kwa picha zilizomwonyesha akimpiga busu mfungwa kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii .

Taarifa iliyotolewa na Idara ya Magereza nchini humo imesema kuwa ilifahamishwa kuhusu picha zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kwamba wakati wanafanya uchunguzi wa tukio hilo, tayari ofisa huyo alikuwa ameshajinyonga.

Aidha, Kamishna wa Magereza wa Limpopo‚ Mandla Mkabela amesema kuwa katika taarifa yao kwamba wameshtushwa sana na wamehuzunishwa mno na tukio hilo la kujinyonga kwa Askari huyo.

“Tumetuma timu ya mameneja waandamizi na wataalamu wa mpango wa ushauri kwa wafanyakazi kwa ajili ya kutoa msaada wowote muhimu,” amesema Mkabela.

Hata hivyo, Mkabela amelaani tukio la usambazaji wa picha zinazodaiwa kuwa ni za ofisa huyo ambazo zimeweza kumsababishia kuchukua maamuzi ya kujinyonga.

 

Mahakama Kuu Kenya yaondoa zuio la maandamano
Majeruhi yazidi kuiandama Chelsea