Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ametangaza kusitisha mpango wa vijana wa chama hicho kwenda Dodoma kuzuia Mkutano Mkuu wa CCM ili kuepusha maafa ambayo yanaweza kutokea.
Mbowe aliwataka vijana hao kutokwenda Dodoma na wawaache CCM waendelee na mkutano wao kwa kuwa Chadema haina hofu na mkutano wa chama hicho.