Mwanamuzi maarufu wa R&B kutoka nchini Marekani August Alsina amethibitisha wazi kuwa katika dimbwi zito la mawazo akitafakari hatma ya maisha yake kiasi cha kuweka bayana kuwa pengine hana matumaini ya kuendelea kuishi zaidi anatafakari juu ya maisha na kifo huku akipambania na afya yake.

Kupitia ukurasa wake maalum wa mtandao wa Instagram, Alsina ameandika ujumbe wa kuhuzunisha na kufichua kwamba anapigania kubaki hai.

“Macho yangu yanaonekana kufungwa, Hapo ndipo ninapoishi, katika hali ya mara kwa mara ya kutumia gps zangu za ndani kuvinjari njia yangu katika nyanja za vita, usaliti, na shaka binafsi wakati kelele inayonizingira ni kubwa sana.”

Lakini maono, yamenipa uwazi kujua kwamba niko kwenye safari yangu kuelekea kifo, na kuwa na amani ya kweli, na ninaposafiri kuelekea huko, uzoefu na mafundisho ya maisha yananihitaji kuacha kila sehemu yangu uwanjani,” ameandika Alsina.

Huku akiendelea kwa kujaribu kujipa moyo kuwa pengine ataishinda hali anayoipitia kwa sasa na kurejea kwenye hali nzuri ya kiafya na kuyafurahia maisha yake kama ilivyokuwa hapo awali.

“BAKI TU AGOSTI!!” Unajua kuwa kinakuja! Unaweza kujua namna ya kujitoa kwenye njia hiyo, ondoa mapepo wabaya, kwa maana huwezi kurudi na kutembelea tena mahali hapa,” ameongeza.

Nyota huyo amekuwa wazi kuhusu vita yake dhidi ugonjwa wa autoimmune, ambao huko nyuma mnamo Julai 2019, aliwahi kudokeza kuhusu wakati wa kutisha uliowahi kumtokea ambapo alijikuta amepooza mwili mzima ghafla kwa muda, jambo lililomlazimu kulazwa hospitalini.

“Siku moja niliamka na sikuweza kutembea, sikuweza kuhisi miguu yangu, na daktari wangu aliishia kunilaza hospitalini,” alisema August, ambaye alikubwa na tatizo la uharibifu wa mishipa kutokana na ugonjwa huo, ambao hutokea wakati mfumo wa kinga ya mwili unapozishambulia seli zenye afya katika mwili binaadamu kimakosa.

Wakati huo alipoweka wazi taarifa za hali mbaya anayoipitia Alsina aliwagusa wengi kiasi cha kupokea maombi kutoka kwa maelfu ya mashabiki wake duniani kote waliweka bayana hisia zao kupitia kurasa za mitandao mbali mbali ya kijamii.

Mwezi uliopita, August Alsina aliachia wimbo wake mpya ‘Shake the World’ ambao alionekana kuzungumzia uhusiano wake uliozungumzwa sana na Jada Pinkett Smith, mke wa mwigizaji maarufu duniani Will Smith.

Habari kubwa kwenye Magazeti leo Mei 10, 2022
Majaliwa:Wabadhirifu MSD wachukuliwe hatua haraka