Si wasanii wote waliofanikiwa kumaliza shule au walimaliza kozi zao wakiwa vyuoni.
Wapo wasanii walioshindwa kufanikisha malengo yao kwenye masomo kwa mfano msaanii dogo janja alishindwa kuhitimu shule wakati anasoma makongo kutokana na kushindwa kufikisha alama za ufaulu. Lakini hii ipo tofauti kwa msanii Ayler anaetamba na kibao cha nenda.
Wengi waliishia njiani kutokana na jinsi chuo hicho kilivyo strict huku wasanii wenye ratiba nyingi za show wakishindwa kufua dafu. Lakini si kwa muimbaji wa Ayler.
Ayler amesema kwenye kipindi cha Chill na Sky kuwa baadhi ya wahadhiri wa chuo hicho wamekuwa na kasumba ya kuwakomalia wasanii wanaosoma hapo wakiamini kuwa wasanii ni watu wa kula bata tu.
“Sometimes walimu wanakutengenezea vikwazo tu upate tu sup uende ukajibebishe lakini no way out I was really studying hard ukikutana na watu nimesoma nao watakumbia kwamba mimi I work so hard. I was really working hard.”
Amesema hadi alipohitimu chuo alimshukuru Mungu. Ayler alihitimu shahada ya Computer Science. Wasanii wengine waliowahi kusoma chuo hicho na kushindwa kumaliza ni Ben Pol, M-Rap na wengine.