Basi kampuni ya Ulamaa T 330 DGB lililokuwa likisafiri kwenda Arusha kutokea Mwanza limepata ajali alfajiri ya leo Juni 30, 2021 kwa kuacha njia na kugonga nyumba eneo la Mkolani darajani Mwanza.

Imeelezwa kwamba ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na Watu 6 ambapo hakuna taarifa za kifo bali Majeruhi tu ambao wamepelekwa Hospitali ya Butimba.

Chanzo cha ajali kinaelezwa kuwa ni baada ya Dereva wa Basi kulikwepa gari dogo kulikosababisha gari kuacha njia baada ya kushindwa kulimudu, taarifa zaidi kukujia.

Mchakato wa katiba unachelewesha maendeleo?
Wapiganaji wa TPLF waonya vikosi vya Serikali