Waimbaji wa Kike wa Bongo Flava, Vanessa Mdee na Shilole wametibuana na kushindwa kuvumilia mipaka ya mgogoro wao na kuamua kuanikana kwenye mitandao ya kijamii.

Bifu hilo ambao limeanza kushika moto wiki hii, limekuwa kavukavu kwani kila mmoja amempost mwenzake kabla ya kumwaga matusi yake.

Ni kama kila mmoja ame-pick the wrong fight, Vanessa wa Uzunguni na Shilole anayejiita wa uswahilini, kila mmoja ana mtindo tofauti wa kumvuruga mwenzake.

Jana, Shilole amepost video na picha kadhaa zinazorusha makombora moja kwa moja kwa Vanessa Mdee akionesha kuwa ameamua kufanya hivyo baada ya kuchokozwa.

“Jaman Vee kaanzisha ugomvi Na wa Igunga ajue tu kuumaliza. Kukauka Kama kuni vepeeee #SayMaName” aliandika Shilole

Jaman Vee kaanzisha ugomvi Na wa Igunga ajue tu kuumaliza. Kukauka Kama kuni vepeeee #SayMaName

A photo posted by Shishi bybee /she roll it (@shilolekiuno_badgirlshishi) on

Veeee jipange Sana mwenzio IGUNGA niliaga cjaletwa kwa kubebwa kwenye Lori nimekuja Na mbio za mwenge. We c wa magorofan Na kingereza chako cha kuunga mi ndo mtoto wa mbwa sasa maninaaaaaaa,” alisema.


Naye Vanessa alishindwa kuvumilia na leo aliamua kurusha kombora akipost picha ya Shilole na kudai kuwa mwimbaji huyo anataka ampe ‘kick ajulikane’. Hata hivyo, Vanessa alidai kuwa Shilole hastahili post hiyo na kwamba angeitoa ndani ya muda mfupi.

“Nikupe KICKIII ujulikane au sio? Kila siku twanyamaza ndiyo mtugaragaze. Sit the f**k down. Mimi sio wale uliowazoea. P.s: You ain’t worth this post inashushwa sasa hivi. #MessageSent” aliandika Vee Money kwenye post aliyoweka picha ya Shilole.

Vee Money

 

Young Africans Kukamilisha Mtihani Wa Afrika Hii Leo
Walioisaliti Simba SC Msimu Wa 2015-16 Watajwa Hadharani