Ndege mpya aina ya Bombardier Q400 iliyonunuliwa na serikali ya Tanzania imeruka kutoka Canada kuelekea Dar es Salaam.

Ndege hiyo ni ya tatu kati ya ndege sita alizoahidi kununua Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dkt. John Magufuli katika juhudi zake za kufufua shirika la ndege la taifa.

Aidha, Ndege aina ya Dreamliner inayoundwa na kampuni ya Boeing inaarifiwa kuwa iko katika hatua za mwisho za kutengenezwa kwa mujibu wa msemaji wa Ikulu.

 

Katibu wa Chadema aachia ngazi, ajiunga na CCM
Mambosasa afunguka muhusika mauaji ya Akwilina