Taarifa iliyotufikia muda huu ni kwamba Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde amefariki dunia leo Machi 7, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amethibitisha kwamba Kibonde amefariki akiwa Mwanza, alianza kusumbuliwa na Presha toka Bukoba kwenye msiba wa Ruge Mutahaba na kuhamishiwa Mwanza.

Aidha, siku chache zilizopita, Clouds Media iliondokewa na mkurugenzi wake wa vipindi, Ruge Mutahaba aliyezikwa nyumbani kwao wilayani Bukoba mkoa wa Kagera.

Dar24 Media inatoa pole kwa CLOUDS MEDIA GROUP.

Mgumba awafunda wakulima wa Pamba
Wauzaji wa Pembejeo wapewa darasa Njombe