Luis Suarez anakaribia kuwa mchezaji bora duniani na kuenguliwa kwake kwenye tatu bora ya Ballon d’Or ilikuwa ni jambo la kushangaza, hiyo ni kwa mujibu wa aliyekua meneja wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers.

Suarez aliuzwa na Liverpool kwenda Barcelona kipindi cha Rodgers mwezi July mwaka 2014 na kuibuka lulu kwenye kikosi cha Luis Enrique kwa misimu miwili iliyopita.

Luis Suarez left Liverpool to join Barcelona, and has become a mainstay in the first team at the Nou CampLuis Suarez aliondoka Liverpool na kujiunga na Barcelona na kuwa moja ya nguzo muhimu ndani ya Nou Camp

Rodgers alimfagilia sana Suarez Jumatatu usiku kwenye mazungumzo yake na Sky Sports, pale alipoulizwa iwapo mchezaji huyo ana nafasi ya kuwa mchezaji bora dunia.

Arsenal Kuchagizwa Na Ujio Wa Majembe Yao
Siri: Kalamu zenye Kamera zilivyowezesha ushindi wa Ukawa Umeya Kinondoni na Ilala