Kiungo kutoka nchini Brazil na Klabu ya Singida Big Stars Bruno Barroso amekanusha uvumi unaoendelea kuhusu mpango wa kusajiliwa na Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans.

Bruno amekua akitajwa sana kuwa kwenye mpango wa kuhamia Young Africans mwishoni mwa msimu huu, kufautia kuonesha kiwango bora tangu alipotua Singida Big Stars.

Akizungumza na Dar24 Media baada ya mchezo dhidi ya Simba SC jana Ijumaa (Februari 03), Kiungo huyo amesema hafahamu lolote kuhusu Young Africans, lakini amekua wakisikia taarifa za kuhusishwa na klabu hiyo ya Dar es salaam.

Amesema anachotambua kwa sasa yeye ni mchezaji wa Singida Big Stars na yupo klabuni hapo kwa misingi na taratibu za mkataba, kwa hiyo hawezi kusema lolote kuhusu mpango huo wa usajili wa kwenda kwingine mwishoni mwa msimu huu.

“Nimejitolewa kuja Tanzania kwa ajili ya kuitumikia Singida Big Stars, ndio maana ninacheza kwa moyo wangu wote na kuisaidia timu kama mnavyoona, sijui lolote kuhusu mpango wa kwenda klabu nyingine.”

“Nimekua nasikia taarifa za mimi kutakiwa Young Africans, lakini ukweli ni kwamba sifahamu lolote kuhusu hilo na ninasisitiza nipo hapa Singida Big Stars kwa mapenzi na nitaendelea kupambana kwa ajili ya klabu hii.” amesema Bruno

CCM yampa siku 14 Waziri Kairuki
Precision Air warudisha shukurani Bukoka