Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) limetangaza gharama za tiketi za kutazama mechi za Fainali za Africa (AFCON) zinazotarajia kuanza mwezi ujao nchini Misri.

Kwa upande wa Shrikisho la soka nchini TFF limethibitisha taarifa hiyo, ikisema kuwa CAF imetangaza gharama hizo kwa madaraja mbalimbali, kwenye michezo ya hatua ya makundi ambayo itahusisha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) tiketi za daraja la kwanza ni USD 29 ambayo ni sawa na takribani sh 66,700 za Kitanzania, tiketi za daraja la pili ni USD 18 ambazo ni sawa na sh 41,403 tiketi za daraja la tatu ni USD 6.

Katika hatua ya makundi, Taifa Stars itacheza michezo mitatu ambapo itaanza dhidi ya Senegal ikifuatiwa na mchezo dhidi ya Kenya na kumalizia hatua hiyo kwa kucheza na Algeria

Aidha, Kwenye hatua ya robo fainali gharama ya tiketi daraja la kwanza ni USD 35 ambayo ni takribani sh 80,521 kwa daraja la pili ni USD 24 na daraja la tatu ni USD 12.

Hatua ya nusu fainali, tiketi daraja la kwanza ni USD 59 ambazo ni sawa na sh 135,700, daraja la pili ikiwa ni USD 29 na daraja la 3 USD 18. Mchezo wa mshindi wa 3 utakua na gharama ya USD 35 kwa daraja la kwanza, USD 24 kwa daraja la 2 na USD 12 daraja la 3.

Mchezo wa fainali, daraja la kwanza ni USD 106 ambazo ni takribani sh 243,800, daraja la 2 ni USD 44 ambazo ni takribani sh 101,200 na daraja la tatu ni USD 24.

Pia TFF imesema kwa yoyote mwenye nia ya kununua tiketi hizo za AFCON awasiliane na shirikisho hilo mapema kabla ya kufungwa kwa muda wa maombi.

Mashabiki waiandalia Futari Kagera Sugar
Membe amjibu Rostam kuhusu kugombea 2020, 'sote tumekatwa mikia'