Chama cha soka nchini England (FA) kimepanga ratiba ya michezo ya mzunguuko wa tatu wa michuano ya kombe la ligi (Carabao Cup) itakayochezwa Septemba 25.

Katika ratiba hiyo majogoo wa jiji Liverpool wamepangwa kucheza na Chelsea, katika uwanja wa Anfield.

Wawili hao watakutana mara mbili mfululizo katika juma moja, ambapo baada ya mchezo huo, Chelsea watawakaribisha Liverpool kwenye uwanja wa Stamford Bridge, kwa ajili ya mpambano wa ligi Septemba 29.

Ratiba hiyo inaonyesha, mabingwa watetezi wa michuano hiyo Manchester City wamapangwa kupambana na Oxford United wanaoshiriki ligi daraja la pili nchini England.

Katika hatua nyingine, meneja Jose Mourinho atakutana kwa mara ya kwanza na mchezaji wake wa zamani Frank Lampard akiwa mkuu wa benchi la ufundi la Derby county kwenye uwanja wa Old Trafford.

Lampard alicheza chini ya utawala wa Mourinho alipokua meneja wa klabu ya Chelsea na kufanikiwa kutwaa taji la ligi ya England mara mbili mfululizo msimu wa 2004/05 na 2005/06.

Washindi wa pili wa michuano hiyo msimu uliopita Arsenal wamepangwa kuanzia nyumbani Emirates Stadium kwa kuwakabili wapinzani kutoka jijini London, Brentford.

Tottenham watakua wenyeji wa Watford, na tayari wameshawasilisha maombi kwenye bodi ya EFL, ili mchezo huo upigwe kwenye uwanja wa MK jijini London.

Everton watacheza dhidi ya Southampton na Wolves watakutana na Leicester City.

Ratiba kamili ya michezo ya mzunguuko wa tatu wa michuano ya kombe la ligi (Carabao Cup).

West Brom v Crystal Palace

Arsenal v Brentford

Burton v Burnley

Wycombe v Norwich

Oxford United v Manchester City

West Ham v Macclesfield

Millwall v Fulham

Liverpool v Chelsea

Bournemouth v Blackburn

Preston v Middlesbrough

Wolves v Leicester

Tottenham v Watford

Blackpool v Queens Park Rangers

Everton v Southampton

Manchester United v Derby

Nottingham Forest v Stoke

Video: Mavoko aachia video ya Ndegele, awakwaruza WCB
Video: Magufuli amshushia nyundo Makonda, Dk. Bashiru atema nyongo