Kutokana na upasuaji wa kuongeza mwili unaojulikana kama (liposuction) alioufanya  rappa Cardi B umesababisha kujitoa kutumbuiza kwenye tamasha la 92Q Spring Bling lilipangwa kufanyika ijumaa hii mjini Maryland.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ rapa Cardi b amejitoa baaada ya kupata tatizo mara tu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongea baadhi ya sehemu za mwili wake.

kwa mujibu wa vyanzo vya karibu vya rapa huyo vimeeleza kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kupona baada ya kufanya pia upasuaji wa maziwa yake.

Hata hivyo Madaktari wameshauri kuwa Cardi B anahitaji mapumziko ya muda mrefu ili mwili wake urudi kama zamani kutokana na baadhi ya sehemu alizofanyiwa upasuaji kuwa hazijapona vizuri.

Imeelezwa kuwa Cardi B alifanya upasuaji huo mara tu baada ya kumpata mtoto wake wa kwanza Kulture, May 5,2019

Aidha Cardi B alisikika akiwaambia mashabiki zake katika tamasha lilofanyika Memphis kuwa alitaka kuahirisha tamasha hilo kwasababu kucheza sana kunaweza kumsababishia matatizo.

Mabweni ya shule ya Wasichana Ashira yateketea kwa moto
Rais Putin apata watoto Mapacha