Chuo cha IFM wametwaa ubingwa wa Ligi ya Vyuo vya Elimu ya Juu mkoa wa Dar Es Salaam baada ya kuishinda Chuo cha Ardhi kwa magoli 6-4 kwenye mchezo wa fainali iliyochezwa kwenye Ufukwe wa Coco Jumapili Januari 7, 2018.
Kufika fainali IFM ilicheza na Chuo cha TIA kwenye mchezo wa nusu fainali ambao walishinda kwa penati 3-2 baada ya kutoka sare ya mabao 7-7.
Ardhi kwenye nusu fainali waliishinda DIT kwa magoli 9-6 ushindi uliowapa nafasi ya kucheza fainali na IFM na kupoteza.
Mchezo huo wa fainali ulilazimika kwenda kwenye muda wa nyongeza baada ya muda wa kawaida timu hizo kumaliza zikifungana magoli 4-4 na katika muda wa nyongeza IFM wakajipatia magoli yao yaliyowapa ubingwa.
Kwenye Ligi hiyo mchezaji Jarufu Juma wa Chuo cha DIT ameibuka kuwa kinara wa mabao akifunga magoli 17

Rais Karia atuma salamu za rambirambi
Moto walipuka Wodini, waua