Daktari mpya wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Sergio Soto Perez, kutoka nchini Hispania ametua nchini leo mchana tayari kabisa kujiunga na timu hiyo.
Mtaalamu huyo wa viungo vya wachezaji alipokelewa na Meneja wa Azam FC, Luckson Kakolaki, aliyeambatana na Kocha Mkuu, Zeben Hernandez.
Perez ataungana na jopo la madaktari wengine wa Azam FC, ambao ni Juma Mwimbe na Twalib Mbaraka, wanaoendelea kutoa matibabu kwa wachezaji wa timu hiyo.
Chanzo: Azam FC