Beki wa pembeni kutoka nchini Brazil Dani Alves, amethibitisha rasmi kuachana na mabingwa wa soka nchini Italia Juventus FC, baada ya kuwatumikia kwa msimu mmoja.

Alves alikua hajasema lolote kuhusu kuondoka kwake mjini Turine, licha ya uongozi wa Juventus kutoa taarifa za kusitisha mkataba na mchezaji huyo waliemsajili akitokea FC Barcelona mwanzoni mwa msimu wa 2016/17.

Alves mwenye umri wa miaka 34, alisaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya Juventus, lakini mwishoni mwa msimu uliopita alianzisha mazungumzo ya kutaka mkataba huo uvunjwe ili atimize melengo aliyojiwekea.

Lengo kubwa linalotajwa kuwa sababu ya kumuhamisha Alves klabuni hapo, ni kutaka kujiunga tena na aliyekua meneja wake alipokua FC Barcelona Pep Guardiola, ambaye kwa sasa anakinoa kikosi cha Man City ya England.

“Ninapenda kuwashukuru watu wote waliofanikisha maisha yangu nikiwa Juventus FC kwa kipindi cha mwaka mmoja, ninawashukuru wachezaji wenzangu tuliocheza kwa ushirikiano mkubwa, tumefanikiwa kwa pamoja mpaka kucheza fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya…,” Alves ameandika katika akaunti yake ya Instagram.

“Leo uhusiano wetu wa karibu unakwisha rasmi, na nitakuwa katika majukumu mengine kisoka, daima nitaendelea kukumbuka mchango wangu nilioutoa nikiwa na Juve, ambayo ni moja ya klabu kubwa nilioitumikia kwa dhati ya moyo wangu.”

Me gustarĂ­a agradecer a todos los TIFOSI DE LA JUVENTUS por el año vivido, A LOS COMPAĂ‘EROS POR ACOGERME Y A LOS PROFESIONALES QUE SON, POR ELLOS QUE ESE CLUB GANA Y LLEGA A FINALES. Creo que mi respecto a ese club y su aficiĂłn fue minha dedicaciĂłn, mi entrega, mi pasiĂłn y todo mi esfuerzo para hacer de ese club, un club más grande cada dĂ­a. Pido perdĂłn a los aficionados de la Juventus si algĂşn momento pensaron que hice alguna cosa para ofenderles, nunca jamás tuve esa intenciĂłn, apenas tengo una forma de vivir las cosas espontáneamente QUE pocos lo entienden… aunque parezca no soy perfecto, pero mi corazĂłn es puro. Hoy finaliza nuestra relaciĂłn profesional y llevarĂ© conmigo todos los que hacen de verdad y de corazĂłn la Juve un grande club. Como saben yo siempre peco por decir lo que pienso y lo que siento…. yo siento que debo decir gracias al señor MAROTA por la oportunidad que te di de tener um grande profesional e alguien que ama su profesiĂłn como el que más…. no juego al fĂştbol por dinero, juego al fĂştbol porque amo essa profesiĂłn y respecto a los que forman parte de ella. Dejare que tu aproveches lo que he trabajado para que tu hagas muchos años de vacaciones. Yo AMO EL FĂšTBOL y dinero jamás va me retener en algĂşn lugar. MUCHAS GRACIAS! #TAMOACTIVOPANITA????

A post shared by DanialvesD2 My Twitter (@danialves23) on

Odinga apiga marufuku ngono siku ya uchaguzi
Chile kuumana na Ureno kombe la mabara, yaahidi kumdhibiti Ronaldo