Mkuu wa wilaya ya Nkasi, Saidi Mtanda amesema kuwa  kama ikibainikika  kuna mwananchi yeyote alipigwa na kuteswa  wakati wa operesheni  ya kuwaondoa wananchi waliovamia na kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya Msitu wa Hifadhi ya Mfili ambayo aliiongoza, atajiuzulu wadhifa huo.

Ameyasema hayo mjini Namanyere Nkasi mbele ya Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula alipokutana na watumishi wa Halmashauri ya Nkasi na kusikiliza kero za wananchi.

“Mimi mwenyewe  ndio niliongoza operesheni hiyo na ninasema hakuna mwananchi yeyote aliyepigwa na kunyanyaswa na ninakiri kuna baadhi ya nyumba ziliteketezwa kwa moto, lakini kama kuna mtu yeyote aliyenyanyaswa na kuonewa niko teyari kujiuzulu mbele ya Naibu Waziri kwa sababu mimi ndio niliongoza zoezi hilo”alisema Mtanda.

Kwa upande wake mbunge wa wa jimbo la Nkasi kusini, Desderius Mipata amesema kuwa malalamiko ya wananchi ni ya kweli kwani Serikali wilani Nkasi ilitumia nguvu kubwa kuwatimua wananchi ndani ya msitu huo.

Hata hivyo Naibu Waziri Mabula, aliipongeza Serikali ya wilaya ya Nkasi kwa opresheni hiyo kwa kuzingatia sheria huku akiwashauri madiwani wafuate  utratibu iwapo kama wanataka  kubadilisha sheria ndogo ya mwaka 1998 inayoeleza kuwa msitu huo umehifadhiwa kisheria.

 

 

Muhongo: TPDC toeni leseni kwa wakati
NEC yapata ugeni kutoka tume za uchaguzi Duniani (AWEB)