Diamond Platinumz pamoja na wasanii wanaounda kundi la Mafikizolo kutoka nchini Afrika Kusini, leo wameingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dododoma.
Wasanii hao wamepata fursa ya kutazama na kusikiliza uwasilishwaji wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Michezo na Wasanii kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016 ikisomwa katika jumba hilo la wawawakilishi.