Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wamepongezwa kutokana na jitihada kubwa za kukuza diplomasia ya uchumi zilizofanyika mwaka 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax akizungumza wakati wa mkutano wake wa kwanza na Watumishi wa Wizara hiyo tangu kuteuliwa kwake kwenye wadhifa huo mwezi Oktioba 2022. Mkutano huo umefanyika jijini Dodoma.

Pongezi hizo zimetolewa jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax wakati wa kikao chake cha kwanza na watumishi wa Wizara tangu kuteuliwa kushika wadhifa huo Oktoba 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax akizungumza wakati wa mkutano wake wa kwanza na Watumishi wa Wizara hiyo tangu kuteuliwa kwake kwenye wadhifa huo Oktioba 2022. 

Ameyataja maeneo ambayo Wizara imeyaratibu kwa ufanisi unaoridhisha kuwa ni pamoja na ziara za viongozi wa kitaifa nje ya nchi, ushiriki wa viongozi katika mikutano ya kikanda na kimataifa, na uandaaji wa mikutano ya Tume za Kudumu za Pamoja za Ushirikiano (JPCs).

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza kumkaribisha Waziri Dkt Tax wakati wa mkutano  na Watumishi wa Wizara hiyo.

Amesema majukumu hayo ambayo sio mepesi kuyatekeleza, yamekuwa na manufaa makubwa nchini katika nyanja za kidiplomasia na uchumi na kuwasihi watumishi kuendeleza jitihada hizo kwa kuzingatia weledi, uzalendo na uadilifu katika kusimamia maslahi ya Taifa.

Mtoto wa miaka 6 ampiga sisasi Mwalimu wake
Mawaziri wawili kuzuru nchini Ethiopia