Mshambuliaji wa klabu bingwa nchini Ufaransa Paris Saint-Germain Edinson Cavani ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mguu wa dhahabu, katika hafla iliyofanyika mjini Monaco.

Cavani ameshinda tuzo hiyo baada ya kukidhi vigezo vyote ambavyo, vinamuwezesha kuwapiku magwiji Cristiano Ronaldo, Luis Suarez na Lionel Messi, ambao walidhaniwa huenda mmoja wao angeibuka kidedea.

Tuzo hiyo ambayo huratibiwa na World Champions Club, hutolewa kwa mchezaji mwenye nidhamu, ushirikiano na msaada mkubwa kwa timu/klabu anayoitimikia, na anapaswa kuwa na umri wa miaka 28 ama zaidi.

Cavani mwenye umri wa miaka 31, alionyesha uwezo mkubwa kisoka msimu uliopota, kwa kuisaidia PSG kutwaa ubingwa wa Ufaransa pamoja na kufika hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa barani Ulaya, kabla ya kutolewa na Real Madrid.

Cavani alianza safari yake ya soka la ushindani akiwa nchini kwao Uruguay katika klabu ya Danubio, kabla ya kutimkia barani Ulaya kujiunga na Palermo ya Italia mwaka 2007.

Image result for Golden Foot AwardTuzo ya mguu wa dhahabu (Golden Foot Award).

Tangu msimu wa 2008-09, amekua akionyesha uwezo mkubwa wa kufunga mabao zaidi ya kumi, akiwa na klabu za Palermo, Napoli, pamoja na mabingwa wa soka nchini Ufaransa (French Ligue 1) PSG, ambapo tayari ameshafanikiwa kutwaa mataji manne.

Cavani pia ameshaifungia timu yake ya taifa mabao 46 katika michezo 106 aliyocheza, na amefanikiwa kutwaa ubingwa wa mataifa ya kusini mwa Amerika (Copa America) mwaka 2011.

Waliokua wakiwania tuzo ya mguu wa dhahabu mwaka huu 2018.

Manuel Neuer (Germany, Bayern Munich), Lionel Messi (Argentina, Barcelona), Cristiano Ronaldo (Portugal, Juventus), Luis Suarez (Uruguay, Barcelona), Edinson Cavani (Uruguay, PSG), Gareth Bale (Wales, Real Madrid), Sergio Ramos (Spain, Real Madrid), Robert Lewandowski (Poland, Bayern Munich), Sergio Aguero (Argentina, Man City) na Thiago Silva (Brazil, PSG).

Waliowahi kushinda tuzo ya mguu wa dhahabu tangu mwaka 2003.

2003  Roberto Baggio  (Italy, Brescia), 2004  Pavel Nedvěd  (Czech Republic, Juventus), 2005  Andriy Shevchenko (Ukraine, Milan)      , 2006  Ronaldo  (Brazil, Real Madrid), 2007  Alessandro Del Piero  (Italy, Juventus), 2008  Roberto Carlos  (Brazil, Fenerbahçe), 2009  Ronaldinho  (Brazil, Milan), 2010  Francesco Totti  (Italy, Roma), 2011  Ryan Giggs  (Wales, Manchester United), 2012  Zlatan Ibrahimović  (Sweden, PSG), 2013  Didier Drogba  (Ivory Coast, Galatasaray), 2014  Andrés Iniesta  (Spain, Barcelona), 2015  Samuel Eto’o  (Cameroon, Antalyaspor), 2016  Gianluigi Buffon  (Italy, Juventus) na  2017  Iker Casillas  (Spain, Porto)

TPDC kuongeza vituo vya kujazia Gesi Asilia
RADO watangaza hukumu ya Mohamed Issa "Banka"