Wachezaji Michael Carrick, Antonio Valencia pamoja na Matteo Darmian wameachwa mjini Manchester, wakati kikosi cha Mashetani Wekundi kiliposafiri kuelekea nchini Ukraine, tayari kwa mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Europa League utakaochezwa hii leo dhidi ya Zorya Luhansk.

Kuachwa kwa wachezaji hao kumetokana na hali zao kiafya kutokua vyema na ushauri ambao ulitolewa na jopo la madaktari umeshinikiza wachezaji hao kuachwa ili wapate muda wa kupumzika.

Kikosi kilichosafiri kuelekea Ukraine yupo De Gea, Romero, Johnstone, Fosu-Mensah, Jones, Bailly, Rojo, Blind, Young, Fellaini, Herrera, Pogba, Lingard, Mata, Mkhitaryan, Martial, Rashford, Rooney na Ibrahimovic.

Kukosekana kwa wachezaji hao kumepokelewa kama changamoto kwa Jose Mourinho kuelekea katika mtanage wa hii leo ambao utakua na umuhimu mkubwa kwa Man Utd.

Man Utd wanatakiwa kushinda mchezo huo ili kujiwe katika mazingira yasiyo na utata ya kusonga mbele kwenye michuano ya Europa League.

Hata hivyo safari ya Man Utd itategemea matokeo ya mchezo mwingine wa kundi lao ambapo Feyenoord ya Uholanzi itakua ikikabiliana na Fenerbahce ya Uturuki.

Endapo Feyenoord watashindwa kuchomoza na ushindi katika mchezo wa hii leo, itakua rahisi kwa Man Utd kusonga mbele hata kama watapoteza mchezo wao dhidi ya Zorya Luhansk.

Michezo mingine ya Europa League itakayochezezwa hii leo.

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI A

Feyenoord v Fenerbahçe

Zorya Luhansk v Manchester United

 

UEFA EUROPA LEAGUE – GROUP B

Apoel Nicosia v Olympiakos

BSC Young Boys v FC Astana

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI C

Mainz 05 v FK Qabala

RSC Anderlecht v Saint-Étienne

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI D

AZ Alkmaar v Zenit St Petersburg

Maccabi Tel-Aviv v Dundalk

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI E

Astra Giurgiu v Roma

Viktoria Plzen v Austria Vienna

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI F

Sassuolo v KRC Genk

Rapid Vienna v Athletic Bilbao

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI G

Panathinaikos v Celta Vigo

Standard Liege v Ajax

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI H

Konyaspor v KAA Gent

Sporting Braga v Shaktar Donetsk

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI I

FC Red Bull Salzburg v FC Schalke 04

Nice v FK Krasnodar

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI J

FK Qarabag v Fiorentina

PAOK Salonika v Slovan Liberec

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI K

Inter Milan v Sparta Prague

Southampton v Hapoel Be’er Sheva

 

UEFA EUROPA LEAGUE – KUNDI L

Osmanlispor v FC Zürich

Villarreal v Steaua Bucharest

Roy Hodgson: Ninajihisi Vizuri Zaidi Kuliko Nilivyokua
16 Bora Za Mabingwa Ulaya Zajulikana