Mashetani wekundu Man Utd wamepangiwa kukutana na klabu ya Midtjylland ya nchini Denmark, katika hatua ya 32 bora ya michuano ya Europa League.

Man Utd wameangukia kwenye michuano hiyo baada ya kutupwa nje kwenye mshike mshike wa Champions League hatua ya makundi.

Katika droo iliyopangwa muda mchache uliopita, ilitarajiwa huenda Man Utd wangepangiwa kigogo katika michuano hiyo lakini sasa inatazamiwa huenda ikawa ni mteremko kwao, kutokana na uzoefu mkubwa walionao tofauti na Midtjylland.

Kwa upande wa majogoo wa jiji, Liverpool wanaoendeshwa na meneja Jurgen Klopp watakutana na klabu kutoka kutoka nchini Ujerumani Augsburg.

Tottenham Hotspur wao wamepelekwa nchini Italia kupambana na Fiorentina.

Ratiba ya hatua ya 32 bora ya Europa League iliyotokana na droo iliyochezeshwa muda mchache uliopita huko mjini Nyon nchini Uswiz ni kama ifuatavyo.

Valencia v Rapid Vienna

Fiorentina v Tottenham Hotspur

Borussia Dortmund v FC Porto

Fenerbahce v Lokomotiv Moscow

Anderlecht v Olympiakos

Midtjylland v Manchester United

Augsburg v Liverpool

Sparta Prague v Krasnodar

Galatasaray v Lazio

Sion v Braga

Shakhtar Donetsk v Schalke

Marseille v Athletic Bilbao

Sevilla v Molde

Sporting Lisbon v Bayer Leverkusen

Villarreal v Napoli

Saint-Etienne v Basel

TFF Yavikumbusha Vilabu Kuheshimu Na Kufuata Taratibu
Ni Arsenal Vs Barcelona Hatua Ya 16 Bora