Baadhi ya klabu za ligi kuu ya soka nchini England, zimefahamu wapinzani wao katika mzunguuko wa pili wa michuano ya kombe la ligi EFL Cup (English Football League).

Klabu za Liverpool, Chelsea pamoja na Everton ni sehemu ya klabu shiriki za ligi kuu ya soka nchini England ambazo zitaanza kuonekana katika mzunguuko wa pili wa michuano hiyo.

Liverpool watapambana na Burton Albion ugenini, Chelsea watakuwa nyumbani wakimsubiri mshindi wa mchezo kati ya Bristol Rovers na Bristol City huku Everton watapapatuana na Yeovil katika uwanja wa Goodison Park.

Liverpool walifahamu mapema kama wangecheza mchezo huo ugenini kutokana na ombi lao kupokelea vyema na chama cha soka nchini England FA, kufuatia matengenezo ya jukwaa kuu ambayo yatakuwa yakifanyika mwishoni mwa mwezi huu katika uwanja wa Anfield.

Kikosi cha Jurgen Klopp kitalazimika kucheza kwa malengo makubwa ili kurekebisha makosa yao ya msimu uliopita, baada ya kushindwa kumaliza vyema kwenye mchezo wa hatua ya fainali dhidi ya Manchester City, ambao walichomoza na ushindi wa mikwaju ya penati.

Michezo ya mzunguuko wa pili wa michuano ya kombe la ligi EFL Cup (English Football League), imepangwa kuchezwa Agosti 23 na 24, na ratiba kamili inayonyesha kuwa:

QPR v Rochdale

Scunthorpe v Cardiff/Bristol City

Watford v Gillingham

Peterborough v Swansea

Everton v Yeovil

Millwall v Nottingham Forest

Sunderland v Shrewsbury

Luton v Leeds

Chelsea v Bristol Rovers/Bristol City

Burton v Liverpool

Blackburn v Crewe

Accrington v Burnley

Crystal Palace v Blackpool

Morecambe v AFC Bournemouth

Preston v Oldham

Oxford v Brighton

Reading v MK Dons

Fulham v Middlesbrough

Newcastle v Cheltenham

Exeter v Hull City

Derby v Carlisle

Northampton v West Brom

Wolves v Cambridge

Stevenage v Stoke

Norwich v Coventry

Frank de Boer Azima Moto Kwa Petroli, Abisha Hodi Stadio San Paolo
Adnan Januzaj Achukizwa Na Falsafa Za Mourinho