Barcelona wametwaa taji la tano katika michuano mbalimbali iliyoshiriki mwaka 2015 baada ya kuifunga River Plate ya Argentina mabao 3-0 na kunyakua taji la Dunia ngazi ya vilabu.
Mchezo huo wa fainali ulifanyika mchana wa leo huko nchini Japan.
Barcelona ameshiriki fainali hizo akiwa ni bingwa wa Ulaya ngazi ya vilabu.
Mabao matatu ya Barcelona yamefungwa na Messi (36′), Suárez (49′, 68′).Katika mchezo huo, River Plate walionekana kushindwa kuimudu safu ya ushambuliaji ya Barca iliyoongozwa na Lionel Messi.