Shirikisho la soka duniani FIFA limemtimua naibu katibu wake, Markus Kattner kwa kujihusisha na ukiukwaji wa matumizi ya siri ya mamilioni ya dola.

Kattnet raia wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 45 alikua akiitumikia nafasi hiyo baada ya aliyekua katibu Jerome Valcke kutimuliwa kazi kutokana na kashfa za rushwa.

Kufutwa kazi kwa kiongozi huyo kulikuja mara moja baada ya bodi ya uchuguzi ya ndani ya Fifa kugundua kulikua na ukiukwaji na uvunjaji wa majukumu yake.

Kulikuwa na ushahidi wa kutosha kuonyesha mapungufu katika majukumu yake kwa kutumia pesa za ziada ambazo waliamua kiasi gani rais, katibu mkuu na naibu katibu mkuu walipwe.

Katika siku za karibuni viongozi waandamizi wa shirikisho hilo wamekutwa na tuhuma za rushwa akiwemo aliyekuwa kiongozi mkuu Sepp Blatter.

Usajili Wa Zlatan Ibrahimovic, Man Utd Kutumia Kivuli Cha Mourinho
MAJALIWA AKUTANA NA KAGAME, WATANZANIA WAISHIO ZAMBIA - PICHA