Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro sasa itaondoka nchini siku ya jumapili usiku kuelekea Istambul nchini Uturuki kwa kambi ya siku nane kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria Septemba 05, 2015.

Awali Taifa Stars ilikua ipitie Muscat nchini Oman kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya nchi hiyo, lakini kutokana na shirkikisho la Soka la Oman kushindwa kukidhi mahitaji ya Kanuni za FIFA za uuandaaji wa mechi ya kimataifa ya kirafiki sasa mchezo huo hautakuwepo tena.

Stars inatarajiwa kuondoka jumapili usiku na shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines) na kuwasili Istambul (Ataturk Airport) siku ya jumatatu majira ya saa 5 kamili asubuhi, kisha kuelekea Kocael katika hoteli ya Green Park Kartepe ambapo ndio itakua kambi yake ya wiki moja.

Saanya Akabidhiwa Jukumu Zito Jumamosi
Malinzi: Tupo Tayari Kwa U17 2019