Kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu zina hamasa ya aina yake huku kila kambi ikihakikisha hailiachi jiwe lolote la upande hasimu bila kugeuzwa.

Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema ameukejeli uamuzi wa CCM kumchagua Wema Sepetu kuwa mwenyekiti msaidizi wa kampeni ya chama hicho ya ‘Mama Ongea Na Mwanao’, yenye lengo la kuwashawishi akina mama kuwaambia watoto wao waichague CCM.

“Hivi kwa nini watanzania tunadanganywa mchana kweupe na akina Wema Sepetu na wenzake, eti wameanzisha kampeni inaitwa ‘mama ongea na mwanao’, hivi kweli kuna mtu asiyejua tabia na mienendo ya Wema Sepetu ilivyo!? Sasa ataongeaje na watoto wetu,” alisema Lema kwenye mkutano wa Kampeni uliofanyika wilayani Karatu.

Wema Sepetu ni mwenyekiti msaidizi wa kampeni ya Mama Ongea na Mwanao ya CCM, iliyo chini ya uenyekiti wa Steve Nyerere.

Dogo Janja Azawadiwa Gari Kwenye ‘Birthday’
Ronaldo Akandamiza Tatu Champions League