Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amesema kuwa hakuna kazi ngumu kama kuteua viongozi au kutengua.

Ameyasema hayo Ikulu jijini Dar es salaam katika hafla ya kuwaapisha Mawaziri na Manaibu waziri, ambapo amewataka viongozi hao kwenda kufanya kazi kwa bidii.

“Unajua hakuna kazi ngumu kama kuteua na kutengua, tunampa kazi kubwa sana Rais wetu, kwa hiyo niwaombe viongozi mlioteuliwa makachape kazi,”amesema Ndugai

Makampuni 15 yajitokeza kununua Korosho
Steve Nyerere adai kutishiwa kuuawa