Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, Mkoani Pwani imetenga kiasi cha sh. bil 5.3 kwa ajili ya ujenzi wa makao makuu ya wilaya hiyo.
Â
Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Yusufu Mbinda wakati akizungumzia baadhi ya utekelezaji wa masuala ya miundombinu ya maji, chakula na mifugo.
Â
Amesema kuwa wametenga mil. 969.1 zitakazotumika katika ujenzi wa daraja la Mwake lenye urefu wa mita 40 ili kurahisisha mawasailiano ya njia ya barabara .
Â
Aidha, ameongeza kuwa wakandarasi wanafanya utafiti wa vyanzo vya uchimbaji visima katika vijiji mbalimbali lengo likiwa kuwaondolea kero ya ukosefu wa maji wananchi.
Â
Hata hivyo, Mbinda amevitaja baadhi ya vijiji vinavyotarajia kunufaika na mpango huo kuwa ni Nyamisati, Mtunda, Mchungu, Mahege na Kivinja A.
Â
-
Makonda kupitia upya taaluma za wanasheria, asimamisha kesi zote
-
Video: Makonda awatumbua wakuu wa Idara za Ardhi
-
Makonda nusura aue mtu Jijini Dar