Mwanamitindo Hamisa Mobetto ambaye ni mama mtoto wa Diamond Platinumz amefunguka kupitia ukuraasa wa Instagram wa Baba mtoto wake, Diamond Platinumz mara baada ndugu wa msanii huyo kuongea maneno yaliyoonesha kumkejeli.

Kufuatia maneno hayo ambayo yamezagaa katika mtandao wa Instagram Hamisa ameibuka na kuandika waraka mzito akimtaka Diamond Platinumz kuoa mwanamke ambaye ndugu, maneja na mashabiki wa Diamond wanamtaka aoe kwani katika andiko lake ameonesha kukerwa na baadhi ya maneno yaliyoongelewa katika mitandao ya kijamii kuhusu yeye mara baada ya wimbo wa Iyena kutoka.

Ambapo katika wimbo huo Diamond ameonekana akifunga ndoa na aliyekuwa mpenzi wake na mama watoto wake Zarinah Hassan.

”Ndo uoe huyo mwanamke ambae anatakiwa na ndugu na manager zako bila kusahau mashabiki, sio kutwa mie mtoto wa watu naandamwa na kukaliwa mie kooni!!! sijakuita wala kukufunga kamba, kila siku maneno mimi kwani alishindwa kukufata kukushauri mpaka akimbilie kwenye matv na mitandaoni ?. Ameandika Hamissa.

Mobeto amefunguka hayo kufuatia post mbalimbali zilizokuwa zikitumwa na watu wa karibu wa Diamond Platinumz wakidai kuwa wamemkumbuka sana Zari hivyo wanataka arudi ili ndoa iweze kufungukika.

Wimbo wa Iyena pamoja na mistari yake umewaibua watu wengi na mashabiki wengi ambao wameonekana kumshambulia kwa maneno mwanadada Hamisa Mobetto.

Hamisa amtaka Diamond kuifunda familia yake..'waambie waheshimu damu yako'
Rais Magufuli apandisha cheo maafisa 9 magereza