Hospitali ya Wilaya ya Siha iliyopo mkoani Kilimanjaro imetatua tatizo kubwa la upatikanaji wa dawa lililokuwa linaikabili hospitali hiyo na kusababisha wagonjwa kuhangaika kutafuta huduma hiyo katika maduka mbalimbali ya watu binafsi, huku dawa hizo zikiuzwa kwa bei kubwa tofauti na ya hospitalini hapo.
Akizungumza hivi karibuni  kwa njia ya simu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo Bw. Andrew Method, alisema ni kweli hospitali hiyo ilikua na uhaba mkubwa wa dawa hali iliyosababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa lakini zimefanyika jitihada kadhaa na kwa sasa hospitali hiyo imetatua tatizo hilo kwa asilimia 70.
“Tayari tulishaagiza dawa, na nyingi tulizokosa Bohari Kuu ya Dawa, tuliziagiza kutoka kwa wazabuni na tunatarajia kuzipata kabla ya mwisho wa wiki hii kwa ajili ya matumizi ya wagonjwa wanaokuja kutibiwa katika hospitali yetu na tunaamini zitasaidia kupunguza tatizo kwa asilimia 70 alisema Bw. Method

Aliongeza kuwa, waliagiza dawa za aina mbalimbali ikiwemo za “antibiotics” na za kutuliza maumivu pamoja na vifaa tiba ambapo vyote kwa pamoja vimegharimu fedha  kiasi  cha shilingi milioni 10.
Aidha, Bw. Method alisema kuwa hospitali hiyo imeandaa mikakati kadhaa ili  kuhakikisha tatizo hilo linapatiwa ufumbuzi wa kudumu, ambapo  tayari wanajindaa na taratibu za kufanya  manunuzi ya dawa kutoka katika Bohari Kuu ya Dawa ikiwa ni pamoja na jitihada mbalimbali zinazofanywa kwa kushirikiana na  Mkuu wa Wilaya hiyo

Raisi Magufuli Amteua Dkt.Modestus Kipilimba Kuwa Kuwa Mkurugenzi Mkuu Idara Ya Usalama Wa Taifa
Watumishi Wizara Ya Habari Watakiwa Kuwa Wabunifu Kiutendaji