Wakati Waislamu wote duniani wanaendelea kufanya ibada na toba katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Idris Sultan ametoa maoni yake kuhusu wale wanaopost kwenye mitandao kile wanachokula nyakati za jioni baada ya muda wa kufunga (iftari).

Idris ameeleza kile anachoamini kuwa lengo la mfungo wa Ramadhani na namna bora zaidi ya kufuturu, huku akisisitiza kuwa kutubu na kutoa shukurani kwa wasio nacho ndio njia bora.

Aliwakosoa wale wanaowapa mialiko rafiki zao pekee kwenye futari zao badala ya kuwaalika zaidi wasiojiweza na watu masikini.

Msanii huyo alisisitiza kuwa lengo la ujumbe wake ni kuwakumbusha waumini wa dini ya Kiislam jinsi bora ya kuweza kupata dhwawabu za Mungu, kwa kufuturisha.
Huu ndio ujumbe wake:

Chadema waelezea mazingira ya kifo cha ghafla cha Ndesamburo, mwili kuchunguzwa
Manchester United klabu ghali kuliko zote barani Ulaya