Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, Amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC Bw. Boniventure Baya kumuandikia hati ya zuio ya muda wa siku saba mkurugenzi wa kampuni ya Maji safi na Maji taka jijini DarEs Salaam na Pwani DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja ya  Kueleza kwa nini kampuni hiyo imetelekeza miundombinu yake ya majitaka na kupelekea uchafuzi wa mazingira katika jiji la Dar Es Salaam.

Akitoa  Agizo Hilo Jijini Dar Es Salaam Mwishoni mwa mwiki wakati wa majumuisho wa ziara yake ya ukaguzi wa viwanda, mazingira na miundombonu ya DAWASCO na DAWASA, NAibu Waziri Mpina alisema hati hiyo itamtaka Mkurugenzi huyo wa DAWASCO kueleza kwa nini kampuni hiyo haitibu  maji yatokayo viwandani huku ikiendelea kupokea fedha toka viwandani na kuachia maji kusambaa katika makazi ya watu.

Mpina Aliongeza kuwa DAWASCO wamekuwa wakipita katika viwanda mbali mbali nchi na kutoza fedha za uzalishaji maji taka bila kuyapima maji hayo na kuelekeza katika miundo mbinu mibovu.

Katika ziara hiyo ya siku nne, Naibu Waziri aligundua kuwa miundombinu mingi ya DAWASCO iko katika hali mbaya, huku walinzi wa miundo mbinu hiyo wakifanya kazi katika mazingira hatarishi kwa afya zao kwa kukosa vifaa vya kujikinga akitolea mfano kituo cha ku pump maji taka cha gymkhana kinachopeleka maji taka katika bomba kubwa la majitaka baharini.

“Hati hiyo atakayoandikiwa mkurugenzi wa DAWASCO itamtaka atueleze kwa nini hali ya miundombinu ipo hivi, kwa nini hawayatibu maji yanayotiririka kwa wananchi huku wanapokea fedha toka katika viwanda, na kwa nini wanatiririsha maji taka katika mto msimbazi bila kuyapima.” Alisema Mh.Mpina

Akitolea Mfano kiwanda cha Sadoline kinachotengeneza Rangi, alisema kiwanda hicho kimekuwa kikiwalipa DAWASCO zaidi ya shilingi milioni moja kwa mwezi kwa ajili ya huduma ya uondoshwaji wa maji taka kupitia miundombinu ya DAWASCO.

Aidha alisema katika kiwanda cha kutengeneza vinywaji laini cha AZAM kilichopo vingunguti, DAWASCO imekuwa ikipokea zaidi ya shilingi milioni tatu kwa mwezi kwa ajili ya huduma hiyo lakini DAWASCO wamekuwa wakipitisha maji hayo katikati ya makazi ya watu na kwenda kuyatitirisha katika mto msimbazi jambo ambalo kisheria ni kosa.

“Hakuna huduma yoyote ya kutibu maji inayofanywa na DAWASCO huku wamekuwa wakiendela kupokea pesa katika viwanda, miundombinu yao ni mibovu, mabwawa ya kuhifadhia maji taka yamekuwa yakitirirsha maji hayo katika makazi ya watu, kiukweli nahitaji maelezo ya kutosha kutoka DAWASCO.” Alisema Mpina.

Kwa upande wake Mratibu wa mazingira wa kanda kutoka NEMC Bw. Jaffari Chimgege alisema kuwa kutokana na ubovu wa miundombinu ya DAWASCO hali ya jiji la Dar Es Salaam imekuwa chafu.

Alisema kunahitajika kazi ya ziada kurekebisha miundombinu hiyo kwani hali hii ikiendelea wananchi watakuwa hatarini kupata magonjwa hivyo ni lazima kazi ya ziada ifanyike.

“Inatupasa kila mtu kjutimiza wajibu wake kwa watu wa viwanda,wananchi na DAWASCO kuhakikisha maji yanayotiririka yanakuwa yamepimwa na kuonyesha kama hayana madhara yoyote kwa binadamu na sio kuacha maji taka kutirirka katika makazi ya watu, hii ni hatari tunahatarisha afya za watanznaia.” Alisema Chimgege.

Nae Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mji mpya kata ya Mnyamani, bw. Rahim Gassi alisema anaishukuru serikali kwa kutembelea mataa wake kwani maji taka  yamekuwa yakititiririshwa na kusababisha watu kupata magonjwa.

Alisema Maji taka hayo yanayotirirshwa katika mto msimbazi ndiyo maji yanayomwagiliwa mambogamboga na wakulima kasha kuwauzia watuwatu hali ambayo si nzuri ki afya.

Manji Awavua Uanachama Wajumbe Watatu Yanga
Serengeti Boys Waivimbia Afrika Kusini