Rapa Joh Makini ameeleza sababu zilizomfanya ajiweke kando na kampeni za siasa kama msanii kwa kufanya shows kwenye mikutano ya kampeni.

Rapa huyo ameeleza kuwa heshima yake kwa mashabiki wa itikadi zote na dini zote ndio sababu kubwa inayomfanya aache kujiunga na kampeni hizo ili asiwatenganishe.

“Nina mashabiki kutoka vyama vyote, vile vile nina mashabiki kutoka dini zote, kwahiyo najaribu pia kuepuka kuwatenganisha,” aliiambia Clouds FM.

Hata hivyo Joh Makini aliongeza kuwa wasanii walioamua kufanya kampeni hawajakosea kwa kuwa wako kazini na wanafanya biashara.

“Kwa sababu mimi kama msanii ni mfanyabiashara end of the day ukinilipa hela yangu, nije ni perfome nyumbani kwako sebuleni au kwenye kampeni yako, mimi nikija pale nitafanya yangu na mwisho wa siku hao wanaopiga kelele, hawajui kwamba hakuna mtu anaweza kukataa kufanya kazi yake akilipwa. Mwisho wa siku kama mtu ameenda kufanya show na amelipwa hela yake hiyo ni haki yake,” Joh alifafanua.

Amir Khan Aendelea Kumuota Floyd Mayweather
Hii Ni Habari Njema Kwa Shabiki Wa ‘Empire’