KIUNGO mkabaji wa Simba, Jonas Mkude amesema anafurahi kuendelea kuweka rekodi ya kuwa mchezaji anayeshiriki matamasha mengi ya Simba Day ndani ya timu hiyo.

Mkude amefunguka hayo kuelekea siku ya Simba Day inayotarajiwa kufanyika Agosti 8 mwaka huu, Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.

Kupitia mtandao wa kijamii Instagram ameandika kuwa ‘Agosti 8 tunaadhimisha Simba Day ya 14 kwangu mimi binafsi ni ya 12,”

“Ni heshima kwangu kuwa sehemu ya tamasha hilo kubwa la soka kwa miaka yote hiyo, tukutane kwa Mkapa kuadhimisha siku yetu wanasimba,” ameandika Mkude.

Habari kuu kwenye magazeti ya leo Julai 27, 2022
Maagizo ya Nape Taasisi za Serikali