Hatimae kiungo kutoka nchini Hispania Juan Mata ameanza kupata mwangaza wa maisha yake chini ya utawala wa meneja wa Man Utd Jose Mourinho, kufuatia hatua ya kuwa katika mazungumzo ya kusaini mkataba mpya.

Mata ambaye alikua sehemu ya kikosi cha Hispania kilichotwaa ubingwa wa dunia wakati wa fainali za kombe la dunia za mwaka 2010, ameonyesha kuwa tayari kubaki Old Trafford na kucheza soka la ushindani kwa vitendo.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28, kwa sasa bado ana mkataba wa miaka miwili ambao unamuwezesha kulipwa mshahara wa Pauni 130,000 kwa juma, na kama mambo yatakwenda vyema kiasi hicho fedha kitaongezeka.

Mata ambaye aliwahi kucheza soka akiwa na klabu ya Valencia kabla ya kuelekea nchini Uingereza kujiunga na Chelsea na kisha Man Utd, alionekana kuwa adui mkubwa wa Jose Mourinho na ujio wa meneja huyo ulitazamwa kwa jicho la tatu kwa kuamini huenda ulikua mwisho kwa kiungo huyo.

Mourinho amethibitisha kuendelea kwa mazungumzo baina ya uongozi wa Man Utd dhidi ya mchezaji huyo na wakati wowote mambo huenda yakakaa sawa.

“Kuna mazungumzo yanaendelea kati yake na uongozi, na nina matarajio makubwa ya kuona jambo hilo likifanikiwa.

“Ameonyesha nia ya dhati ya kutaka kubaki hapa kwa vitendo kutokana na kutumia nafasi ya kucheza soka safu kwa kufuata maelekeo anayopewa wakati wote. Alisema Mourinho

Mata alionyesha umahiri mkubwa wakati wa mchezo wa ligi ya Uingereza mwishoni mwa juma lililopita dhidi ya mabingwa watetezi Leicester City kwa kuitendea haki namba 10.

Jose Mourinho alipokua Chelsea alishindwa kwenda sambamba na Juan Mata na kufikia hatua ya kumuuza Old Trafford.

Aubameyang Akoleza Moto Wa Usajili
Video: Dk. Kijo Bisimba amshauri Rais JPM kufuata misingi ya katiba, utawala wa sheria