Tamasha lililopewa jina ‘ONE LOVE’ limefanyika jijini Manchester ili kuwafuta machozi wahanga wa tukio la kigaidi lililotokea kwenye Manchester mnamo tarehe 22 Mei 2017.

Takribani watu 50000 wamehudhuria onyesho hilo lililofanyika wiki mbili baada ya shambulio la kujitoa muhanga lililoua watu 22 nakujeruhi watu wengine zaidi ya 100 muda mchache baada ya onyesho la mwanamziki Ariana Grande kumalizika.

Aidha, tamasha hilo lilihudhuriwa na wasanii waliofanya onyesho hilo ni pamoja na Ariana Grande, Justin Bieber, Coldplay, Katy Perry, Miley Cyrus, Liam Gallagher, Pharrell Williams, Take That, Niall Horan, Little Mix, Robbie Williams na Black Eyed Peas.

? Live Breakingnews: Hukumu ya Ester Bulaya, Halima Mdee Bungeni.
ACT-Wazalendo kwafukuta, wamtaka Anna Mghirwa kukataa uteuzi