Kadinali Laurent Monsengwo, aliyekuwa mkosoaji wa utawala wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila amejiuzulu ikiwa ni wiki chache kabla ya nchi hiyo kufanya uchaguzi mkuu.

Monsengwo mwenye umri wa miaka 79, ambaye pia alikuwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki la Kinshasa, amemuachia Fridolin Ambongo nafasi hiyo.

“Papa Francis leo ameridhia ombi la Kadinali Laurent Monsengwo. Fridolin Ambongo atachukua nafasi yake,” msemaji wa kanisa hilo la Kinshasa, Bruno Lusongakio amekaririwa na AFP.

Ukosoaji wa wazi na ukali wa Monsengwo dhidi ya utawala wa Rais Kabila uliodumu kwa zaidi miaka mingi, unahusisha pia mauaji ya waandamanaji.

Mwanzon mwa mwaka huu, Kadinali huyo alijihusisha na uratibu wa maandamano ya kupinga hatua za Rais Kabila kuvuka ukomo wa muhula wa urais uliwekwa kwenye Katiba. Maandamano hayo yalifanyika siku moja kabla ya sherehe za siku ya Mwaka Mpya.

Muda wa Rais Kabila kukaa madarakani kwa mujbu wa katiba ulipaswa kukoma mwaka 2016, lakini aliendelea kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kuweka sawa hali ya kiusalama wa nchi kabla ya kuitisha uchaguzi.

Hatua hiyo ilipingwa vikali na vyama vya upinzani pamoja na viongozi wa dini ambao kwa nyakati tofauti waliitisha maandamano. Taifa hilo litafanya uchaguzi wa kidemokrasia kumpata mrithi wa Rais Kabila Disemba 23.

Amber Rutty apandishwa kizimbani, alalamika 'naumwa'
Prince wa Saudi Arabia adai mwandishi aliyeuawa alikuwa hatari