Mke wa mwanamuziki maarufu nchini Marekani, Kanye West amekuwa na matukio ya aina yake katika tasnia ya fasheni na muziki pia itakumbukwa mwaka 2007 utabaki kuwa mwaka wa kukumbukwa kwa Kim kardashian baada ya video ya ngono kuvuja mitandaoni akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Ray j na kumpatia umaarufu mkubwa hadi sasa huku wengi wakibaki na maswali mengi kwa nini wawili hao walichuku uamuzi wa kurekodi video hiyo na kuipandisha mtandaoni.

”Sikuwa katika utimamamu wangu wa akili kwani nilikuwa nimetumia madawa ya kulevya kupita kiasi,” amesema hayo wakati wa mazungumzo na Scott Disisk na Kendall Jenner jana kwenye onyesho la keeping up with the  Kardashian,

Kim alirekodi video hiyo akiwa na umri wa miaka 27, na ilimpatia umaarufu na huku akiwa kimya kwa muda bila kutoa sababu za kufanya hivyo kwa mashabiki wake.

Aidha, amesema kuwa alishafunga ndoa yake ya kwanza kabla ya kuwa na Kanye West, alishawahi kufunga ndoa na mtayarishaji wa Muziki, Damon Thomas huku akiwa hayupo katika utimamu wake wa akili kwa utumiaji wa dawa za kulevya zilizomfanya afanye vitu visivyo eleweka.

 

 

Nyuki wamshambulia kikongwe hadi kufa
HapoKale: Tumkumbuke waziri wa kwanza wa mambo ya ndani nchini Sir George