Mzunguko wa tatu wa michuano wa Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) unatarajiwa kuendelea wikiendi hii mpaka katikati ya juma lijalo kwa michezo 13 kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini.

Kesho Jumamosi michezo mitatu itachezwa, mjini Morogoro Burkinfaso FC watawakaribisha Simba SC katika uwanja wa Jamhuri mjini humo,  Pamba FC watawakaribisha Toto Africans uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, huku Ndanda FC wakichea dhidi ya Mshikamno FC katika uwanja wa Nagwanda Sijaona Mtwara.

Jumapili michuano hiyo itaendelea kwa michezo mitatu, jijini Dar es salaam Young Africans watawakaribisha Friends Rangers uwanja wa Taifa, Njombe Mji watakua wenyeji wa Tanzania Prisons uwanja wa Amani Njombe, huku Stand United wakicheza dhidi ya Mwadui FC katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Michuano hiyo itaendelea Jumatatu, Kagera Sugar wakiwa wenyeji wa Rhino Rangers katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora, Panone FC dhidi ya Madini FC uwanja wa Ushirika mjini Moshi na Africa Lyon wakiwa wenyeji wa Azam FC uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Jumanne Mtibwa Sugar watawakaribisha Abajalo FC uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, Lipuli dhidi ya JKT Ruvu uwanja wa Wambi Mafinga, Africa Sports dhidi ya Coastal Union Mkwakwani jijini Tanga, na Geita Gold watakua wenyeji wa Mgambo Shooting katika uwanja wa Nyankumbu mjini Geita.

Singida United watacheza dhidi ya Mvuvuma siku ya Jumatano katika uwanja wa Namfua mjini Singida, na mchezo wa mwisho utachezwa Februari Mosi katika ya Wenda FC dhidi ya Mbeya City uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Mpaka sasa timu ya JKT Mlale pekee ndio imeshafuzu kwa mzunguko wa nne baada ya kuiondosha Majimaji kwa mabao 2-1, katia mchezo uliochezwa wiki iliyopita kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Ashanti Utd Yaondolewa Kombe La Shirikisho
TFF Yatuma Salamu Za Rambirambi Klabu Ya Tanzania Prisons