Korea Kaskazini na Kusini zimekubaliana kufanya mazungumzo ya kijeshi ili kuondoa wasiwasi uliopo mipakani baada ya mkutano wa kwanza katika kipindi cha miaka miwili.

Ujumbe wa Korea Kaskazini umepinga ajenda ya kusitisha mpango wake wa majaribio ya silahaza kinyuklia uliowasilishwa na Korea Kusini.

Aidha, pande zote mbili zimetoa taarifa ya pamoja ambayo ilithibitisha kuwa wamekubaliana kufanya mazungumzo ya kijeshi ya kuondoa wasiwasi uliopo.

Hata hivyo, taarifa hiyo imesezungumzia kuimarisha uhusiano wa mataifa hayo mawili kulingana na chombo cha habari cha Korea Kusini cha Yonhap.

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba aagiza wenye mimba kukamatwa
Video: Siri kikao cha JPM na Lowassa Ikulu, Mpasuko mkubwa Chadema