Kiingilio cha chini cha mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika kwa Wanawake kati ya timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake ‘Taifa Stars’ dhidi ya timu ya taifa ya wanawake Zimbambwe kitakua shilingi elfu mbili tu.

Mchezo huo namba 3, unatarajiwa kuchezwa siku ya Ijumaa saa 10 kamili jioni katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, huku kiingilio cha juu kikiwa shilingi elfu tatu kwa jukwaa kuuu.

Waamuzi wa mchezo huo ni Lidya Tafesse, akisaidiwa na Yehuzewdubizua Yehuw, Tsige Sisay, Woinshetkassaye Abera kutoka nchini Ethiopia, huku Kamisaa wa mchezo huo Geneviev Kanjika akitoka Congo DR wote wanatarajiwa kuwasili siku ya Alhamisi mchana kwa shirika la ndege la Kenya (KQ).

Wakati huo huo kikosi cha Twiga Stars kimeendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo huo wa siku ya Ijumaa, huku kocha mkuu wa timu hiyo Nasra Juma akisema vijana wake wote wapo katika hali nzuri na tayari kuwakabili Wazimbambwe.

Aidha Kocha Nasra amewaomba wadau wa mpira wa miguu nchini na watanzania wote kwa ujumla, kujitokeza uwanjani siku ya Ijumaa kuja kuwapa sapoti katika mchezo huo, ambapo watakua wakiwakilisha na kupeperusha bendera ya Tanzania.

Serikali yalitaka gazeti la 'Dira ya Mtanzania' kumuomba radhi Sefue kwa kumuita 'jipu'
Majambazi wauawa, wakutwa na ujumbe wa ‘Kova’