Waziri wa michezo wa Ufaransa, Thierry Braillard amebainisha kuwa mechi za Ligi Kuu ya nchi hiyo maarufu kama Ligue 1 na ligi daraja pili au Ligue 2 zinatarajiwa kuendelea kama zilizopangwa mwishoni mwa wiki hii, wiki moja baada ya mashabulio ya kigaidi jijini Paris. 

Mwishoni mwa wiki iliyopita ratiba kadhaa za michezo ndani na maeneo mengine kuzunguko mji huo zilisimamishwa kufuatia matukio hayo ya kigaidi ambayo yamepeleka vifo vya zaidi ya watu 129. 

Kufuatia kikao cha kati ya wizara ya mambo ya ndani na Bodi ya Ligi ya nchi hiyo, Braillard amesema waliafikiana kuwa mechi za ligi za mwishoni mwa wiki hii ziendelee kuchezwa kama zilivyopangwa.

Kikubwa kitakachofanyika katika mechi hizo ni kuongeza hali ya usalama katika maeneo yote ya nchi hiyo ili kuhakikisha hakuna tukio lingine linatokea.

Kuelekea Game Ya El Classico, Ulinzi Waimarishwa Mjini Madrid
Mrembo Akutwa Na Majanga Haya Alipoenda Kukutana Na Mwaume Aliyemfahamu Facebook