Ligi Daraja la Kwanza nchini (StarTimes First League) inaendelea wikiendi hii kwa makundi yote matatu kucheza, michezo 11 itachezwa mwishoni mwa wiki siku za Jumamos na Jumapili katika viwanja mbalimbali nchini.

Jumamosi Kundi A, Ashanti United watakua wenyeji wa Mji Mkuu (CDA) katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, KMC watawakaribisha Polisi Dodoma katika uwanja wa Mabatini – Mlandizi.

Kundi B, Lipuli FC watawakaribisha Polisi Morogoro katika uwanja wa Wambi mkoani Iringa, Kimondo FC watakuwa wenyeji wa JKT Mlale kwenye uwanja wa CCM Vwava – Mbozi, huku Burkinafaso ya Morogoro ikiwakaribisha Njombe Mji katika uwanja wa Jamhuri.

Kundi C, JKT Kanembwa watakuwa wenyeji wa Panone FC katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, JKT Oljoro watawakaribisha Polisi Moro uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Geita Gold watacheza na Rhino Rangers uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita na Polisi Tabora watawakaribsiha Mbao FC mjini Tabora uwanja wa Ali Hassa Mwinyi.

Ligi hiyo itaendelea siku ya Jumapili kwa michezo miwili ya Kundi A, Friends Rangers watacheza dhidi ya African Lyon uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, na Polisi Dar watakua wenyeji wa Kiluvya FC katika uwanja wa Mabatini Mlandizi.

Mzunguuko Wa Tano Ligi Kuu Kuendelea
Taifa Stars Yaanza Kujifua Dar es salaam