Raundi ya saba ya Ligi Daraja la Pili nchini (SDL) inaendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa nchini, kwa timu 24 kusaka pointi kutoka makundi ya A,B,C na D kuwania nafasi nne za juu ili kuweza kupanda ligi daraja la kwanza msimu ujao.

Kundi A, Leo Ijumaa Abajalo Tabora watakua wenyeji wa Mvuvumwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Green Warriors dhidi ya Singida United uwanja wa Mabatin Mlandizi (jumatatu) na Mirambo FC watacheza dhidi ya Transit Camp siku ya jumatatu uwanja wa Ali Hassani Mwinyi mkoani Tabora.

Kundi B, Kesho Jumamosi AFC ya Arusha watakua wenyeji wa Alliance Schools uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Madini FC watacheza dhidi ya JKT Rwamkoma uwanja wa Mbulu, huku Bulyanhulu FC watawakaribsiha Pamba FC uwanja wa Kamabrage mjini Shinyanga.

Kundi C, Leo Ijumaa Abajalo Dar watacheza dhidi ya Mshikamano uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, kesho Jumamosi Kariakoo FC watawakaribisha Changanyikeni katika uwanja wa Ilulu – Lindi, na Cosmopolitani watacheza dhidi ya Villa Squad siku ya jumatatu katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Kundi D, Jumamosi Mighty Elephant watacheza dhidi ya Wenda FC uwanja wa Majimaji mjini Songea, Mbeya Warriors watawakaribisha Mkamba Rangers uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, huku Jumapili Sabasaba FC wakicheza dhidi ya African Wanderers uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Guss Hiddink Amedhihirisha Anachokifanya Chelsea
Soka La China Laanza Kutishia Amani Ya Biashara Ya Wachezaji